Thursday, July 16, 2015
STRESS AU MSONGO WA MAWAZO
3:12 PM
| Posted by
MWAFRIKASILI
|
MSONGO
WA MAWAZO (STRESS)
Msongo wa mawazo ni tatizo la kisaikolojia litokanalo
na mwitikio wa mwili kutokana na jambo fulani linakukabili kwa wakati huo.Kwa
kawaida mwili wa binadamu unapokutana na changamoto yoyote hujiandaa namna ya
kukabiliana nayo au huunda mbinu ya kulikimbia tatizo/changamoto husika.Katika
mchakato huu wa kutafuta majibu mfumo wa mwili huachia homoni mablimbali
ikiwemo Adrenaline ambayo hupelekea
kuongezeka kwa kiwango cha sukari katika mzunguko wa damu hivyo kuathiri mfumo wa kinga mwilini. Msongo
wa mawazo unaweza kukufanya ushindwe kufanya shughuli zako za kila siku kwa
ufanisi au kupata magonjwa kama vile Mgandamizo mkubwa wa damu (BP) au
kuongezeka kwa glokos mwilini
Msongo
wa mawazo huathiri pia mfumo wa akili ya binadamu hivyo hupunguza uwezo wa
kufikiri,hupunguza uwezo wa kukumbuka na mpangilio mzima wa kumbukumbu katika
ubongo hii hupelekea watu wengi kupata magonjwa kama vile stroke au magonjwa
mengine yafananayo na hayo hasa yale yasababishwayo na msawazo mbaya wa homoni
mwilini.
Msongo
wa mawazo wa mawazo ni jambo la kawaida na ni jambo la kila siku katika maisha
ya binadamu.Msongo wa mawazo husababishwa na mambo mabalimbali kama vile;
ü Matukio
makubwa katika maisha kama vile kutalikiwa,kupata mimba isiyotarajiwa,kufeli
mitihani,kifo cha Yule tumpendaye sana au mtu wako wa karibu,kufukuzwa kazi n.k
ü Matukio
ya kila siku kama vile changamoto za kazini kwako (biashara,shambani,ulipoajiriwa
nk)
ü Changamoto
za kimazingira
ü Magonjwa
Hayo ni baadhi tu ya mambo yasababishayo Msongo wa mawazo.Ukweli ni kwamba msongo
wa mawazi kudhibitiwa ili usifikie kiwango cha kuleta madhara, leo nimechambua
baadhi ya mambo ambayo yanaweza kukuwezesha kudhibiti msongo wa mawazo.
1. Weka Malengo yanayotimizika
Binadamu tuna uwezo na sababu
tofauti juu ya malengo tunayo jiwekea.Hata uwezo wa kufikia malengo pia
hutofautiana hivyo, unapoweka malengo
yako hakikisha unazingatia uwezo wako na muda ulionao ili kuweza kuyafanikisha.
Kamwe usiige malengo ya watu wengine bila kupima rasilimali ulizonazo katika
kufikia malengo hayo, daima zingatia uwezo wako ili malengo yako yaweze
kufanikiwa na kuepuka kupata msongo wa mawazo.
2. Tazama tatizo kama
Changamoto wala si kikwazo
Katika maisha huwa tunakutana na
mambo ambayo hatukutaka kukutana nayo na pia tunashindwa kupata yale
tuliyoyataka, karibu kila mtu huwa anapitia hali hii kwa namna moja au
nyingine. Jifunze kukabili matatizo yako kama changamoto na sio kama mlima
mkubwa usiopandika. Jaribu kukubali mambo kwa busara zaidi, na utulivu huku ukitafakari
nini cha kufanya ili kulipata lile ulilo kusudia. Changamoto iwe ni chachu ya
wewe kuzidi kukazana na kujaribu zaidi.
3. Ondoa hofu katika
kila jambo unalotaka kulifanya
Hofu na wasiwasi hukupelekea kutokufanya
maamuzi sahihi katika muda sahihi hii yaweza kukusababishia msongo wa mawazo.
Uwe na ujasiri wa kuamua mara baada ya kutafakari pande zote kwa makini na
kuona faida na hasara za kila upande. Usihofu sana juu ya kuweza kufanya makosa
hadi ukaishia kupata msongo wa mawazo, mara nyingine watu hujifunza kutokana na
makosa.
4. Kutana na wataalam (Wanasaikolojia
au washauri nasaha)
Pale unapokutana na jambo ambalo
umeshindwa kulitatua ni vyema ukamshirikisha mtaalam na ikibidi mzazi wako au mlezi, rafiki
wa karibu au mume/mke. Jifunze kutokuweka mambo yanayokuumiza moyoni maana
katika hali hiyo ni rahisi sana kupata msongo wa mawazo.
5. Kula chakula bora kwa
wakati
Mara nyingi tunakuwa na shughuli
nyingi kiasi cha kusahau kula ,na hata inapotokea tunakula ni ili kukidhi njaa
tu wala si mahitaji halisi ya mwili . Ni muhimu sana mwili wako upate chakula
chenye virutubisho bora na pia unakunywa maji ya kutosha.
6. Fanya mazoezi
Fanya mazoezi ya viungo mara kwa
mara na pata muda wa kutosha wa kupumzika kila siku kila unapojisikia una
msongo wa mawazo .
Hayo aliyojadiliwa hapo ni sehemu tu ya utatuzi wa
msongo wa mawazo.Watu wengi hutumbukia katika gharama za matibabu na wadawa
bila kujua wanatibu nini maana huenda katika hospital mbalimbali napengine
huambiwa “HATUONI UGONJWA” kama nawe ni mmoja wao tafadhali wasiliana nasi
tutatue shida yako.
Tafuta hapa
Kuhusu sisi
Karibu kwenye Blog hii, naamini hautatoka bure na wala hautajuta kuitembelea Blog hii. Karibu sana
Habari Maarufu
-
Code of ethics/code of conduct The term code of ethics and code of conduct have been used interchangeably by teachers and organizatio...
-
TAMBUA MUDA WA KUISHA MATUMIZI YA TAIRI ZAKO Tairi za gari/ pikipiki zinamuda maalumu wa matumizi hivyo ni muhimu sana kujua muda ha...
-
In most communities, there has been, and there still is, a deeply embedded conviction that, under proper conditions, people can help ot...
-
Da da huyu hana mikono lakini mambo anayo yafanya naamini hata wewe lazima ushange
-
K weli huyu mbunifu wa jengo hili anastahili pongezi za dhati. Kwa kuwa jengo ni imara pamoja na kunyeshewa na mvua nyingi halijawah...
Blog Malimbali
All rights reserved by Mwafrikasili - Blog design by ARM's pRo. Powered by Blogger.
Tafsiri
Hati Miliki
© 2013 Mwafrikasili
0 Maoni:
Post a Comment